TESDO MAKAO MAKUU TABORA

tesdo makao makuu

Usajili utafanyika kwa vituo vitatu, TABORA,DODOMA na DAR ES SALAAM, unatakiwa kudownload fomu kwenye blog ya asasi na kuijaza vyema, kisha unatakiwa ulipie ada ya uanachama na fomu kama inavyojieleza kwenye hiyo fomu. Akaunti no 01522250952400. Kwa kituo cha TABORA utakabidhi fomu yakokwa Mohamed Mapalala 0715449745, DODOMA Zahoro HM na Malale Buluba 0764492146. DAR ES SALAAM Mayasa Mzelela 0785314908, kasha baada ya muda utapatiwa risiti yako. Fomu inapatikana sehemu ya TESDO DOCUMENTS. Kwa maoni kuhusu utaratibu tuma kwenye email tesdo@rocketmail.com au simu 0716555450/0785314908.

Hamisi Masoud Mtwale

Mwenyekiti TESDO



Friday, February 10, 2012

Historia ya Mkoa wa tabora

Mkoa wa Tabora chimbuko lake ni mji wa Tabora ambao ulianzishwa katika nusu ya kwanza ya karne ya 19 na wafanyabiashara Wakiarabu na Waswahili kutoka Zanzibar. Waliutumia mji huu kama kituo cha njia ya biashara kati ya Pwani na Ziwa Tanganyika. Biashara kuu ilikuwa ya pembe za Ndovu na Utumwa. Mji wa Tabora ulijengwa kwa nyumba za miti na udongo pamoja na ghala za bidhaa kwa ajili ya biashara. Familia ya Tippu Tip ilikuwa kati ya wenye nyumba za mji wa Tabora.

Mwaka 1871 lilishambuliwa Jeshi na la Rugaruga Wajerumani mji wa Mtemi kuharibiwa  Mirambo kwa kiasi kikubwa, lakini haikuchukuwa miaka mingi, mji huu ukajengwa upya. Wajerumani walipowasili Tabora waliwakuta wanyamwezi(kabila) kubwa likiwa na tawala mbalimbali za kitemi a (chiefdoms).

CHANZO: TAARIFA YA MIAKA HAMSINI (50) YA UHURU WA TANZANIA BARA
                   MKOA WA TABORA
Bofya hapa kupakua taarifa yote....




0 comments

Post a Comment