AJENDA
- Ufunguzi
- Kujadili, kupitisha na kutafutia pesa project ya elimu shule za sekondari
- Mengineyo
Ufunguzi
Mwenyekiti bwana Hamisi Masoud Mtwale alifungua kikao kwa kumuomba Frank Minazi ambaye ni mjumbe kwa kuomba Mwenyezi Mungu abariki kikao chetu mnamo saa 9 mchana.
Kujadili ,kupitisha na kutafutia pesa mradi wa asasi wa elimu shule za sekondari
Wajumbe wakamati walijadili na kupitisha kufanywa mradi huo kisha kuutafutia pesa ikiwa ni pamoja na kuupeleka kwenye vituo mbalimbali vya redio na kuona watu mabalimbali wenye nia njema na Tabora kwa ajili ya kuchangia. mradi huo unajumuisha kumuisha kuchagua shule 14 za mfano yaani 2 kutoka kila wilaya(Tabora mjini, Nzega, Ulyankulu,Urambo,Igunga,Sikonge,Uyui) ili kusaidia mapungufu yake ya madawati,vitabu na kujitolea kufundisha.masomo yaliyopewa kipaumbele ni physics,chemistry,geography,english,mathematics na biology na kutoa elimu kwa uma kuhusu dhana halisi ya kusoma shule. Pia wajumbe walikubaliana kusomesha wanafunzi 49 wasio na uwezo nao ni 7 kutoka kila wilaya miaka minne yaani kidato cha kwanza -cha nne kwa kulipa ada na kutoa michango ya shule na kuwanunulia sare pamoja na madaftari. Pia katika kujitole akufundisha wajumbe walichangia kuwa watu 84 wenye uwezo wa kufundisha masomo ya kipaumbele wajisajili kwenye fomu yetu iliyopo kwenye blog ,watu hao watapangiwa shule hizo na kupewa hela ya kujikimu kwa miezi miwili. Pia watafanyiwa semina ya siku moja Tabora mjini kabla ya kwenda kufundisha.wakiwa wengu zaidi kipaumbele watapewa wenye fani ya elimu (Education). Bajeti kwa makisio ya mwanzo ilikuwa shilingi 156,759,000.
Mengineyo
Wajumbe waliimizana kuendelea na upendo na mshikamano, na zaidi kupambana kwa halina mali katika kuunusuru mkoa wao wa kihistoria.
Kufunga kikao
Mwenyekiti alifunga kikao hicho mnamo saa 12 jioni kwa kumuomba Mungu awazidishie nguvu, afya na kutekeleza miradi ya asasi.
…………………………………….. …..……………………………..
Hamisi Masoud Mtwale Mayasa Mzelela Kazala
Mwenyekiti-TESDO Katibu-TESDO
0 comments
Post a Comment