TESDO MAKAO MAKUU TABORA

tesdo makao makuu

Usajili utafanyika kwa vituo vitatu, TABORA,DODOMA na DAR ES SALAAM, unatakiwa kudownload fomu kwenye blog ya asasi na kuijaza vyema, kisha unatakiwa ulipie ada ya uanachama na fomu kama inavyojieleza kwenye hiyo fomu. Akaunti no 01522250952400. Kwa kituo cha TABORA utakabidhi fomu yakokwa Mohamed Mapalala 0715449745, DODOMA Zahoro HM na Malale Buluba 0764492146. DAR ES SALAAM Mayasa Mzelela 0785314908, kasha baada ya muda utapatiwa risiti yako. Fomu inapatikana sehemu ya TESDO DOCUMENTS. Kwa maoni kuhusu utaratibu tuma kwenye email tesdo@rocketmail.com au simu 0716555450/0785314908.

Hamisi Masoud Mtwale

Mwenyekiti TESDO



Monday, May 28, 2012

TAARIFA FUPI YA SEMINA


UTANGULIZI
Namshukuru Mungu kwa uwezo aliotupa Viongozi na Wana TESDO wa kuwatumikia vyema wana Tabora.Pia shukrani za dhati ziende kwa watendaji wa CG FM radio,VOT Radio na Mhe.Mstahiki Meya wa Manispaa kwa mchango wake wa TSH.50,000/=.
URATIBU WA SEMINA
Semina ya kuwaelimisha wanafunzi walio maliza kidato cha 6 na 4 iliratibiwa chini ya Uongozi wangu na wajumbe wa TESDO BW.Seifu Kazuge,Cassian Puis na Mansoor Juma tangu tarehe 21/05/2012 ofisini makao makuu Tesdo.Aidha mikamati ya kujitolea ilifanywa na majukumu kugawiwa wajumbe wote.

                                                 TESDO OFISIN-viongozi kwakiratibu Seminar

Cassian Puis alijitolea kutengeneza tangazo kwa gharama zake-TSH.100,000/=,Katibu Mtendaji nilisimamia mambo yote yahusuyo Stationaries na Seif alifuatilia Ukumbi na maandalizi yake.wajumbe wengine wakafanya zoezi ya uhamasishaji mahudhurio.
SEMINA KUFANYIKA
Mnamo tarehe 26/05/2012 saa 2.00 asubuhi wajumbe NA VIONGOZI WA TESDO waliwasili eneo la ukumbi wa SAUT/mihayo school.
Vongozi TESDO wakisubiri wajumbe wa semina-UKUMBI WA CHUO CHA SAUT TABORA
Wajumbe wa semina walitarajiwa kuwa wengi sana kwa matangazo tuliokuwa tumetoa kwa vyombo vya Redio lakini haikuwa hivyo kinyume na matarajio yetu.Lakini imani yetu ni kuwa mwanzo mgumu na harakati hizi za kubadili mitazamo na ujanja wa kutumia fursa zinazopatikana ni suala la lazima.Hali ilikuwa hivi
                       Ni wajumbe wachache sana aliohudhuria semina hii


Lakini TESDO na viongozi ake wanaamini katika harakati ya kubadili tabia na mtazamo si jambo lahisi kiasi hicho;hivyo basi kwa kuzingatia rasilimali zilizotumika kuandaa ukumbi ilitupasa kufanya semina kwa wajumbe hawa na kufikisha lengo ili tuwe na wachache wenye nguvu na sio wingi wa povu la sabuni. Semina ikaanzaa;mada zikaanza tolewa.
Mada ya kwanza: Nafasi ya wasomi kusaidia maendeleo ya Mkoa wa Tabora


Wawasilishaji mada TESDO MAKAO MAKUU-aliesimama ni SEIF(kushoto),katikati M.Mapalala na (kulia) ni mjumbe Cassian Pius.

Pamoja na hayo;mada zote zilizopangwa kuhudhurihshwa zilitolewa na wajumbe wakapata kile walicho tarajia kupata.
Mada ya pili: MFUMO WA ELIMU TANZANIA NA FURSA ZA KIELIMU.


                               Mwasilishaji: Mohamed Mapalala

Mada ya Tatu: MAISHA YA CHUO NA CHANGAMOTO ZAKE
                                Mwasilishaji: Mansoor Juma


VIBURUDISHO NA VINYWAJI :
Pamoja na umaskini tuliokuwa nao haikuwa ngumu kufanya makoo yetu safii kwa kutoa mada na kuuliza maswali;



                               wajumbe wakisikiliza mada na kuburudika soda na maji

         Meza ya wawezeshaji –TESDO MAKAO MAKUU

MCHANGANUO WA MATUMIZI
Tulipata fedha toka vyanzo vifuatavyo;

  •  Meya manispaa-50,000/=
  •  Cassian-100,000/=
  •  Mapalala 50,000/=
  •  Utawala SAUT Tabora -200,000/=

JUMLA:400,000/=

Mchanganuo huu ni kwa fedha (gharama) ila Fedha taslimu ilikuwa ni TSH.50,000/= tu.Zinginezo ni huduma zilizotolewa na wahusika kwa gharama hio.
MATUMIZI


Kutengeneza JINGO(TANGAZO)-100,000/=

  •  Kulitangaza Tangazo-30,000/=
  •  Kutoa copy na kuandaa semina papers-50,000/=
  •  Ukumbi-200,000/=
  • Soda na maji 10,000/=
MWISHO
Tunatoa tena shukrani kwa wadau wa maendeleo kufanikisha hili kwa asilimia hii ndogo.Aidha tuna amini kwa wakati mwingine tutaweza zaidi.

Taarifa hii imeandaliwa na:
KATIBU MTENDAJI –TESDO
0715449745
mapalala04@gmail.com







0 comments

Post a Comment