TURUDI NYUMBANI TULIPO SIO KWETU
Habari zenu ndugu zangu, ndugu wa asili yangu, niwapendao kwa dhati ya moyo wangu.
Ni wazi kwamba tupo sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi yetu hasa tukitafuta mahitaji yetu na pia ikiwa ni sehemu ya ajira zetu, lazima ukisoma kichwa cha habari utashtuka,kwanini jamaaa amesema turudi nyumbani kwetu.
Binafsi naamini kuna njia mbili za kufika mahali
- Kimwili
- Kifikra
Kwa muda mrefu sasa wasomi, wajasiliamali wakubwa , watu wenye mafanikio, watu wa kawaida na kada mbalmbali kutoka mkoa wa Tabora wamekuwa kimya katika kutoa eidha michango yao ya fikra au ya mali katika kuhamasisha maendeleo ya mkoa wetu.TESDO tunaona sasa ni wakati muafaka wakutoa fikra zetu duni na kuungana katika asasi yetu hii kwani lazima tujue tuna uwezo wa kuchangia katika yale tunayoona ni changamoto za mkoa wetu. WAHENGA WANASEMA MKATAA KWAO MTUMWA.
Ni kweli tulipasahau kwetu, ni kweli tulijivunia sehemu za wenzetu leo tumebaini na kukubali kwa dhati ya moyo wetu na zaidi tunaamini KUTELEZA SI KUANGUKA,
Tutasimama imara kwa kila hali tutajitoa kwa fikra zetu, mali zetu..TESDO TUNAOMBA KILA MTU AICHUKUE KAULI HII NA AIWEKE MOYONI MWAKE KIUTEKELEZAJI.
Sasa tumeisha peleka maombi yetu CRDB ya kufungua akaunti ya asasi na tumeahidiwa twende leo(tar 15/02/2012)
Baada ya hapo kila atakae chukua fomu ya usajili kwa mapenzi yake na mkoa wetu atairuridisha akiwa kalipa gharama za usajili kwenye akaunti ya asasi.
Mungu wetu tulipatenga kwetu na kutukuza kwingine sasa tumekumbuka ni jukumu letu kupapenda kwetu kwani tumelelewa hadi tukapata mafanikio haya SASA TUMEAMUA KURUDI NYUMBANI HUKU TULIPO SIO KWETU
Na Hamisi Masoud Mtwale
Mwenyekiti-TESDO
TESDO NI YETU, TABORA NI YETU NA MAFANIKIO YAKE NI YETU PIA
0 comments
Post a Comment